|
KATIBA
YA UMOJA WA KIZALENDO WA WATANZANIA
(TanzanianCommunity Organization)
I: MADHUMUNI
1.Kusaidiana katika matatizo yanayohusiana na msiba na
kuendeleza shughuli za kitamaduni
II: UANAUMOJA
-
Mtu yeyote anayekubaliana na madhumuni ya Umoja huu
na anayejitegemea (na sio lazima anaishi California)
anaweza kuwa mwanaumoja.
-
Kutakuwa na kiingilio cha dola ishirini na tano
($25.00). [Wale ambao walishakuwa Wanaumoja kabla ya
tarehe kumi na sita, mwezi wa pili (Februari), mwaka
wa elfu moja mia tisa tisini na sita (2/16/1996)
hawatahitajika kulipa kiingilio hicho].
-
Mwanaumoja anatoa mchango dola kumi ($10.00) kila
mwezi, Mwanaumoja akitaka anaweza kutoa mchango
mpaka mwaka moja (miezi kumi na miwili) kwa wakati
mmoja na sio zaidi.
-
Mwanaumoja anategemewa kuhudhuria mikutano ya
Umoja.
-
Mwanaumoja ambaye hatatoa mchango wake kwa muda wa
miezi mitatu mfululizo atakuwa na siku tano za ziada
kulipa. Mwanaumoja huyo atakubushwa kwa simu au
barua au mjumbe wa Kamati ya Utendaji kabla ya siku
hizo tano kufika. Kama hatakuwa amelipa katika muda
huo ataeleweka kuwa amejitoa kuwa amejitoa na
hatatambuliwa na umoja.
-
Mwanaumoja ataruhusiwa kujinga tena (bila kutoa
kiingilio upya), ikiwa atatoa malimbilikizo ya
michango yote kwa wakati mmoja, na pia atalipa miezi
mitatu ya mbele.
-
Ikiwa mwanaumoja atataka kurejea katika umoja baada
na mwaka moja ( miezi kumi na miwili) au zaidi,
itambidi alipe malimbikizo yote pamoja na kutoa
kiingilio upya.
-
Ikiwa mwanaumoja atapoteza
mapato ( kama kupoteza kazi) na anajiona kuwa hawezi
kuendelea kotoa mchango, itabidi aitaarifu Kamati ya
Utendaji. Uanaumoja wake utalindwa hata baada ya
miezi mitatu. Hata hivyo baada ya hali yake kimapato
kutengamaa, atawajibika kulipa malimbilikizo yake
yote.
III. UTAWALA
Kamati ya Utendaji itakuwa na wanakamati wane (4) kamati
ya utendaji ndiyo itakayoongoza shughuli za kila siku za
umoja.
Wanaumoja watatu (3) watachaguliwa kila baada ya miezi
mitatu, na kazi yao itakuwa ni kusaidiana na wajumbe wa
kamati ya utendaji katika shughuli mbalimbali za Umoja.
1.
A) Shughuli zote za umoja zitaongozwa na kutekelezwa na
wajumbe saba (7)-yaani wajumbe wane (4) wa kamati wa
Utendaji, na wajumbe watatu (3) watakaochaguliwa kila
baada ya miezi mitatu (3).
B)
Kila mjumbe wa kamati ya Utendaji atahudumia kwa muda wa
miaka miwili.
2.
Mjumbe wa kamati ya utendaji akiachia kazi yake kwa
kujitoa, kwa ugonjwa, au kwa kutolewa, nafai
iliyowazi itajazwa na mjumbe atakayechaguliwa na
wanaumoja wote. Lakini iwapo mjumbe huyo wa Kamati ya
Utendaji ni mwenyekiti, katibu, au Mweka Hazina, hapo
wajumbe wanaobaki, watajichagulia Mwenyekiti, Kaimu
Mwenyekiti, Mweka Hazina, au Katibu ipasavyo.
3.
Wajumbe wa kamati ya utendaji hawatalipwa au kupokea
malipo ya aina yeyote kutokana na uongozi wao. Lakini
wajumbe wa kamati ya utendaji wanaweza kurudishiwa fedha
za binafsi walizotumia kw niaba au kwa ajili ya Umoja.
Wajumbe wa kamati ya utendaji hawatakuwa na mkataba na
Umoja, au kuwa na kazi y akulipwa na Umoja.
4.
Ni lazima theluthi mbili (2/3) za wajumbe wa kamati ya
Utendaji au wajumbe watano (5) wa kamati ya utendaji
wawepo ili mkutano wa kamati hiyo utambulike kuwahalali.
5.
Wajumbe wa kamati ya utendaji wakipenda, au
wakikubaliana, au wakiona ni vyema,
Mwanaumoja yeyote wa umoja wa kizalendo anaweza kuwa
mwenyekiti wa shughuli za Umoja wa Kizalendo za
uzalishaji fedha (ukuzaji wa mfuko wa Umoja, n.k.).
6.
(A) Taratibu za Uchaguzi – Kabla ya Uchaguzi
(i)
Mkutano wa uchaguzi utakuwa na wanaumoja watu (3), ambao
sio wajumbe wa Kamati ya Utendaji, kuongoza uchaguzi.
(ii)
Katika mkutano huo wanaumoja watapendekeza majina ya
wagombea nafasi za kamati ya utendaji. Kila pendekezo
ni lazima liungwe na wanaumoja watatu ili jina
lifikiriwe.
(iii)
Mkutano wa uchaguzi utahakikisha kuwa mgombea ambaye
jina lake limependekezwa anakubali kuutumikia umoja kw
amuda wa miaka miwili.
(iv)
Matokeo ya uchaguzi yatatangazwa baada ya kupiga kura na
yatathibitishwa.
(v)
Katiba itakuwa pia katika lugha ya kiingereza, hasa kwa
manufaa ya wanaumoja wasio raia wa Tanzania. Lakini
lugha itakayotumika katika mikutano ni Kiswahili.
(vi)
Kila mjumbe au wajumbe wawili au zaidi wa Kamati ya
Utendaji wanaruhusiwa kuitisha mkutano wa dharura wa
wanumoja wote.
(B)
Siku ya Uchaguzi
(i)
Kamati ya Uchaguzi itatangaza siku ya uchaguzi
(ii)
Kila
mwanaumoja atakuwa na haki ya kupiga kura mara saba (7)
kwa majina tu yaliyopendekezwa kwa nafasi saba.
(iii)
Matokeo ya uchaguzi yatatangazwa baada ya kura zote
kuhesabiwa na kuthibitishwa na kamati ya uchaguzi.
Wshindi saba ndio watakaokuwa wajumbe wa Kamati ya
Uongozi na uchaguzi utakuwa umekamilika.

7.
a. Mwenyekiti au wajumbe wawili au zaidi wa Kamati wa
Utendaji wanaruhusiwa kuitisha mkutano wa dharura wa
wanaumoja wote.
b.
Wajumbe wa kamati ya Utendaji watakuwa na uwezo kuunda
Mwongozo wa umoja kufuatana na mahitaji ya wanaumoja
kwa wakati huo. Marekebisho hayo lazima yawe kwa
maandishi na yawe na sahihi za wajumbe wote wa kamati ya
ya utendaji wa wakati huo.
8.
Mjumbe wa kamati ya uongozi haruhusiwi kushughulika
kikatiba na mwanaumoja kwa niaba ya umoja; anaweza tu
akimbiwa na Kamati ya Utendaji. Mwenyikiti
akisaidiwa na katibu-mweka hazina wanahitajiwa kutoa
taarifa ya hali ya Umoja kifedha na kadhalika, mara moja
kwa mwaka, hasa muda mfupi kabla ya mkutano wa wanaumoja
wote.
9.
Mwenyekiti, akisaidiwa na Mweka Hazina atatoa taarifa ya
fedha za Umoja mara moja kwa mwaka kabla ya mkutano wa
wanaumoja wote.
10.
Mjumbe au wajumbe wa kamati ya utendaji anaweza/wanaweza
kutolewa kwenye kamati kwa sababu au bila ya sababu kwa
jumla ya kura theluthi mbili (2/3) ya wanaumoja wote au
kwa sahihi (petition) kiasi cha theluthi mbili ya
wanaumoja wote au kwa kura tano (5) za wajumbe wa Kamati
ya Utendaji.
11.
Mweka Hazina, au mwanaumoja anayekuwa kama kiongozi
anayeshughulika na zaidi ya dola elfu moja ($1,000)
atatakiwa kuwa na kinga ya kifedha (bond security)kutoka
kwenye kampuni inayoshughulikia masuala hayo. Gharama
zote za “bond” hiyo zitalipiwa na Umoja.
12.
Mjumbe yoyote wa Kamati ya Utendaji atakuwa na haki ya
kukagua vitabu, rekodi, barua ya aina yeyote, na vitu
vyote vya umoja wakati wowote bila kukatazwa.
IV: VIONGOZI
Mwenyekiti
-
Mkuu wa Umoja wa Kizalendo atakuwa Mwenyeki, ambaye
pia atakuwa mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji.
Kadhalika atakuwa mwenyekiti wa mikutano ya
wanaumoja wote.
-
Mwenyekiti ataitisha mikutano yote ya Umoja na ya
Kamati ya Utendaji ya Umoja.
-
Mwenyekiti atatekeleza kazi zote kama ilivyoamuliwa
na Kamati ya Utendaji wakati wakikutana kihalali.
-
Atahakikisha kuwa uamuzi na matakuwa vinatekelezwa
kama ilivyoamuliwa na Kamati ya Utendaji ya Umoja.
Kaimu Mwenyekiti
-
Atachukuwa nafasi ya mwenyekiti iwapo mwenyekiti
hatakuwepo au mgonjwa.
-
Kaimu mwenyekiti atatekeleza kazi kama
itakavyoamuliwa na Kamati ya Utendaji ya Umoja.
-
Iwapo mwenyekiti na kaimu mwenyekiti watashindwa
kutokea kwa ajili ya ugonjwa au vinginevyo, basi
wajumbe wa utendaji watamchagua mmoja kati yao
kushikilia uenyekiti mpaka hapo mwenyekiti
atakapokuwepo.
Katibu
Katika mikutano yote ya Umoja, katibu atachukua maoni
yote na kuyatunza. Atatunza pia rekodi zote za umoja.
Ataandika barua zote za Umoja na kuzituma ipasavyo.
Atatunza orodha zote za wanaumoja, katiba ya umoja na
maelezo yote mengine yahusinavyo na umoja. Kama mjumbe
atashughulika na kazi za Umoja akisaidiana na wajumde wa
Kamati ya Utendaji.
Iwapo katibu atakataa, au ashindwe kutekeleza kazi yake
ilivyoelezwa hapo juu, kazi yake itachukuliwa na
Mwenyekiti au Kaimu wake au mwanaumoja yeyote
atakayechaguliwa na wajumbe wa Kamati ya Utendaji.
Mweka Hazina
-
Kazi yake ni kupokea michango na malipo ya kila
mwanaumoja na kutoa malipo kwa niaba ya Umoja. Pia
atatoa taarifa ya fedha kwenye mikutano au mkutano
wa mwaka wa wanaumoja wote. Yeye pamoja Mwenyekiti
na Kaimu Mwenyekiti ndio pekee wanaoweza kutoa pesa
kutoka benki.
-
Mweka hazina atatunza kwa
ukamilifu malipo yote ya umoja na kutunza stakabadhi
na hundi zote za Umoja.
V: UKAGUZI WA FEDHA
1.
Kamati ya watu watatu (3) itachaguliwa na Kamati
ya Utendaji kutoka miongoni mwa wanaumoja, na itafanya
kazi kama Kamati ya Ukaguzi wa fedha mpa ka kufikia
mkutano wa mwisho wa mwaka wa wanaumoja wote. Mkutano
huo pia utachagua kamati mpya ya ukaguzi wa fedha yenye
idadi ilele ya wajumbe (3). Ikiwa nafasi kwenye kamati
hii itabaki wazi kwa sababu yoyote ile, itajazwa na
mjumbe au wajumbe watakaochaguliwa kwenye mkutano wa
kawaida au wa dharura wa wanaumoja wote. Wajumbe wa
Kamati ya Utendaji ya Umoja hawaruhusiwi kuwa wajumbe
kwenye kmati hii.
2. Baadaye kufuatana na maamuzi
ya Umoja, Umoja unaweza kumwajili mtaalamu mwenye liseni
ya utunzaji na ukaguzi wa vitabu vya fedha, ili aweze
kuwa anafanya ukaguzi wa vitabu vya fedha za Umoja.
Kabla ya kila mkutano wa mwisho wa mwaka, nakala ya
taarifa ya ukaguzi wa fedha itatolewa. Mweka
Hazina atasoma taarifa hiyo kwenye mkutano wa wote wa
mwisho wa mwaka.
VI: MISAADA
1.
Misaada itatolewa kwa ajili ya misiba tu. Ni matatizo ya
msibva tu yatakayohalalisha msaada kutoka kwenye hazina
ya umoja huu kupewa mwanaumoja aliyefiwa na:
a)
Mzazi (baba au mama)
b)
Ndugu wa kuzaliwa naye
c) Ndugu ambaye ni kama mzazi wa mwanaumoja (mzazi
alikufa akiwa mdogo)
d) Mume,
mke au mtoto wa mwanaumoja
2.
a)
Mwanaumoja akifiwa na mtu hapa marekani na anataka
kupeleka maiti nyumbani atasaidiwa kwa kiasi cha
asilimia arobaini (40%) ya fedha za Umoja, lakini kiasi
hiki atachopewa kisizidi dola elfu mbili ($2,000.00) za
Umoja.
b) Mwanaumoja akifiwa na mtu hapa marekanni na hataki
kupeleka maiti nyumbani atasaidiwa kwa kiasi cha
asilimia thelathini (30%) ya fedha za Umoja, lakini
kiasi hiki atachopewa kisizidi dola elfu mbili
($2,000.00) za Umoja.
c) Mwanaumoja akifiwa na mtu nyumbani (nje ya marekani)
na anataka kwenda nyumbani atasaidiwa kwa kiasi cha
asilimia ishiri na tano (25%) yafedha za Umoja, lakini
kiasi hiki atachopewa kisizidi dola elfu moja mia tano
($1,500.00) za Umoja.
d) Mwanaumoja akifiwa na mtu nyumbani (nje ya marekani)
na hataki kwenda nyumbani atasaidiwa kwa kiasi cha
asilimia kumi na tano (15%) ya fedha za Umoja, kiasi
hiki atakachopewa kisizidi dola mia tano ($500.00) za
Umoja.
VII: VITI
VILIVYO WAZI
Ikiwa Mwenyekiti, Kaimu Mwenyekiti, Katibu, au Mweka
Hazina wataacha viti vyao kwa kung’atuka au kwa sababu
yoyote ile, Kamati ya Utendaji itamchagua mwanaumoja
yeyote, au mjumbe wa Kamati ya Utendaji atamchagua
mwanaumoja au mjumbe mwingine wa Kamati ya Utendaji
kushikilia nafasi hiyo iliyowazi kwa muda tu uliobaki,
mpaka uchaguzi mwingine utakapofanyika.
VIII:
UMOJA UKIFA
Umoja ukifa, fedha za Umoja zitagawanywa ifuatavyo:
A)
Kwanza: Umoja utalipa madeni yake yote pamoja na gharama
za kufa kwake.
B)
Pili:
Kila mwanaumoja atarudishiwa fedha kulingana na malipo
aliyoyatoa pamoja na riba kama ipasavyo. Ikiwa fedha
zimetumika kama ilivyoelezwa katika katiba hii, na fedha
zilizobaki hazitoshi kulipa kila mwanaumoja kama
ilivyoelezwa hapo juu hapo basi fedha hizo zitagawanywa
kati ya mwanaumoja kufuatana na makadirio ya wakati
mwanaumoja alipojiunga kwenye Umoja.
IX: NAKALA
YA KATIBA KWA WANAUMOJA
Katiba ya Umoja huu itachapishwa na kila mwanaumoja
atapata nakala yake. Nakala za nyongeza zinazohusiana na
mabadiliko ya kikatiba zitatawanywa kwa wanaumoja pale
zinapokuwa tayari baada ya mabadiliko hayo kufanywa.
Nyongeza hii ni badiliko linalohusu Sehemu II Kipengele
1 cha Katiba hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Wanaouhusiwa kujiunga katika Umoja huu ni kama
ifuatavyo:
Raia
yeyote wa Tanzania au yeyote mwenye asili ya Tanzania,
mke au mume wa Mtanzania, na watoto wa Watanzania.
Uhalai wa badiliko hili ni kuanzia leo Desemba 21,1996.
Inathibitishwa kwamba katika badiliko hili hakuna jambo
lolote linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
2
Nyongeza hii ni badiliko linalohusu Sehemu VI Kipengele
1 cha Katiba hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Umoja huu utafungua akaunti ya kielimu katika benki kwa
ajili ya watoto walioko chini ya umri wa miaka kumi na
minane wa mwanaumoja aliyefariki dunia. Umoja atatoa
mchango wa mara moja utakaowekwa katika akaunti hiyo, na
kiasi cha mchango huo hakitazidi dola mia tatu
($300.00). Uhalali wa badiliko hili ni kuanzia leo Juni
26,1999. Inathibishwa kwamba katika badiliko hili hakuna
jambo lolote linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
3
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu II Kipengele 5 & 7 cha Katiba
hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Mwanaumoja atasimamishwa uanachama ikiwa atashindwa
kulipa ada ya Umoja kwa muda wa miezi ishirini na minne
(24) mfululizo. Mwanaumoja huyo anaweza kujiunga upya
katika Umoja mara baada ya kipindi hicho ikiwa, lakini
atatakiwa kulipa upya kiingilio cha dola hamsini
($50.00). Uhalali wa badiliko hili ni kuanzia leo Machi
24, 2001. Inathibishwa kwamba katika badiliko hili
hakuna jambo lolote linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
4
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu II Kipengele 3 cha Katiba
hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Mwanaumoja atawajibika kulipa ada ya $15.00 kwa mwezi.
Uhalali wa badiliko hili ni kuanzia leo Septemba 29,
2001. Inathibishwa kwamba katika badiliko hili hakuna
jambo lolote linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
5
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu VI Kipengele 3 cha Katiba
hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Kutakuwepo kipindi cha miezi mitatu (3) ambacho
mwanaumoja mpya atasubiri kabla ya kuwa na uhalali wa
kupata msaada wa fedha za Umoja. Uhalali wa badiliko
hili ni kuanzia leo Septemba 29, 2001. Inathibishwa
kwamba katika badiliko hili hakuna jambo lolote
linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
6
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu II Kipengele 5, 6 & 7 cha
Katiba hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Mwanaumoja atasimamishwa uanachama ikiwa atashindwa
kulipa ada ya Umoja kwa muda wa miezi kumi na miwili
(12) mfululizo. Mwanaumoja huyo anaweza kujiunga upya
katika Umoja mara baada ya kipindi hicho ikiwa, lakini
atatakiwa kulipa upya kiingilio cha dola hamsini
($50.00), na pia atalipa ada ya miezi mitatu ya mbele.
Uhalali wa badiliko hili ni kuanzia leo Mei 3, 2003.
Inathibishwa kwamba katika badiliko hili hakuna jambo
lolote linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
7
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu VI Kipengele 2A cha Katiba
hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Ikiwa familia ya marehemu ina zaidi ya mwanaumoja mmoja
katika Umoja huu na ikaamua kumsafirisha maiti nyumbani,
Umoja utatoa asilimia arobaini (40%) ya pesa za
zilizopo, lakini kiasi atakachopewa kisizidi dola elfu
nne ($4,000.00) kwa vile ni kifo kimoja, bila kujali
idadi ya wanaumoja katika familia hiyo. Ikiwa vitatokea
vifo zaidi ya kimoja katika familia moja kwa wakati
mmoja, Umoja utatoa asilimia arobaini (40%) ya pesa
zilizopo kwa kila kifo. Hata hivyo, kitakachotolewa kwa
kila kifo kisizidi dola elfu nne ($4,000.00). Uhalali wa
badiliko hili ni kuanzia leo Mei 3, 2003. Inathibishwa
kwamba katika badiliko hili hakuna jambo lolote
linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
8
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu VI Kipengele 2B ya Katiba
hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Ikiwa mwanaumoja amefiwa na jamaa yake hapa Marekani na
akaamua kumzika hapa, atasaidiwa kwa kiasi cha asilimia
thelathini (30%) ya fedha za Umoja zilizopo, lakini
kiasi hiki atachopewa kisizidi dola elfu mbili
($2,000.00). Ikiwa familia ya marehemu ina zaidi ya
mwanaumoja mmoja katika Umoja huu na familia ikaamua
kumzika marehemu hapa Marekani, Umoja utaipa familia
hiyo nyongeza ya dola elfu moja ($1,000.00). Kiasi hicho
hata hivyo hakitazidi dola elfu tatu ($3,000.00).
Uhalali wa badiliko hili ni kuanzia leo Mei 3, 2003.
Inathibishwa kwamba katika badiliko hili hakuna jambo
lolote linalokiuka Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
9
Nyongeza hii
ni badiliko linalohusu Sehemu VI
ya Katiba hii, nayo ni kama
ifuatavyo:
Umoja huu utaongeza Kipengele 2E cha Sehemu VI ya Katiba
hii. Mwanaumoja akifa na familia yake ikaamua azikwe
hapa Marekani, Umoja utatoa kiasi cha asilimia
thelathini (30%) ya pesa za Umoja zilizopo. Kiasi hiki
hata hivyo kisizidi elfu mbili ($2,000.00). Ikiwa
familia ya marehemu mwanaumoja itaamua kusafirisha mwili
wake nyumbani, umoja utatoa kiasi cha asilimia arobaini
(40%) ya pesa za Umoja zilizopo. Kiasi hicho hata hivyo
kisizidi dola elfu nne ($ 4,000.00). Uhalali wa badiliko
hili ni kuanzia leo Mei 3, 2003. Inathibishwa kwamba
katika badiliko hili hakuna jambo lolote linalokiuka
Katiba ya Umoja.
NYONGEZA:
10
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu II Kipengele 4 cha Katiba
hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Ikiwa mwanaumoja atakosa kuhudhuria mikutano mitatu
(miezi tisa) mfululizo bila sababu muhimu*, atawekwa
katika kipindi cha uangalizi. Ikiwa mwanaumoja atakosa
kuhudhuria mikutano minne mfululizo (miezi kumi na
miwili) bila sababu mihimu, itatambulika kuwa mwanaumoja
huyo amejitoa kwenye Umoja. Uhalali wa badiliko hili ni
kuanzia leo Mei 3, 2003. Inathibishwa kwamba katika
badiliko hili hakuna jambo lolote linalokiuka Katiba ya
Umoja.
NYONGEZA:
11
Nyongeza hii
ni
badiliko linalohusu Sehemu III Kipengele 1A na 1B cha
Katiba hii, nayo ni kama ifuatavyo:
Umoja wa Kizalendo utakuwa na Bodi ya Wakurugenzi. Bodi
hii itakuwa na wajumbe tisa (9) ambao watachaguliwa kila
baada ya miaka miwili. Kuundwa kwa Bodi hii kunaondoa
mara moja nafasi ya wajumbe watatu waliokuwa sehemu ya
kamati ya uongozi, ambao walikuwa wakichaguliwa kila
baada ya miezi mitatu. Uhalali wa badiliko hili ni
kuanzia leo Septemba 27, 2003. Inathibishwa kwamba
katika badiliko hili hakuna jambo lolote linalokiuka
Katiba ya Umoja.
bonyeza
kupata Fomu ya Maombi katika
*
Sababu ya kuwa kazini haiwezi kutolewa zaidi ya mara
moja.
 |