|
| |
Tamko La Lengo La Umoja |
Lengo pana la umoja wetu (Tanzanian Community
Organization) ni kuendeleza nakudumisha umoja wa kitaifa ambao ndio msingi wa
upendo, amani na utulivu katika taifa letu, ambapo madhumuni ya Umoja
kijumuiya ni kujenga jumuiya hai ya Watanzania kwa kuhamasisha
wanajumuiya kujenga uhusiano wa kindugu miongoni mwao, na kuwasaidia
kufikia malengo ya kinafsia na yale ya kijumuiya. Miongoni mwa malengo
hayo ni kama vile kuelewa muundo wa kijamii wa taifa la Marekani,
kufahamu na kufanya mabadiliko muhimu ya
kitamaduni (mila na desturi) nchini Marekani, kujipatia elimu, na jinsi
ya kujiandaa kwa ajira. Sisi kama sehemu ya jamii ya Tanzania iliyoko
mbali na nyumbani, pia tunataka kuchangia maendeleo ya kijamii, kielimu,
na kiuchumi ya Tanzania kwa njia mbalimbali. Umoja wetu pia unapenda
kujenga uhusiano mzuri na jamii nyingine za Kiafrika, vyama mbalimbali
vya kijamii mahali tunapoishi, na jamii nzima kwa jumla kwa vile sisi
pia ni sehemu ya jamii hiyo. Kwa kuhimiza umoja na ushirikiano miongoni
mwa Watanzania hapa Marekani, Umoja wetu unaendeleza umoja wa kitaifa
ambao hulifanya taifa letu kung’aa karibu na mbali. |
|